0


RAIS wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amesisitiza azma ya Serikali ya kuwaongeza mshahara wafanyakazi wa kima cha chini ifikapo Aprili mwaka huu kuwa iko pale pale.
         
      

Akifunga semina ya siku moja kwa Viongozi na Watendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuhusu Umuhimu wa Takwimu na Matumizi yake, katika ukumbi wa Baraza la wawakilishi la zamani, Dkt. Shein amesisitiza kuwa Serikali ipo vizuri na kueleza kuwa ahadi zote zitatekelezwa sambamba na vikosi vya SMZ kulingana kimaslahi na vikosi vyengine.

Pamoja na hayo Dkt. Shein amesisitiza kauli yake kuwataka viongozi na watendaji katika sekta ya umma kuacha kufanya kazi kwa mazoea amesema kuwa ni jukumu la kila kiongozi kubadilika katika utendaji wake wa kazi.
Dkt. Shein amesema tangu alipoingia madarakani mwaka 2010 Zanzibar imepiga hatua kubwa katika ukusanyaji wa mapato na kuchangia kuongezeka takriban mara nne.

Nae Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd amesisitiza haja ya kuwepo kwa mashirikiano katika utoaji wa takwimu na kuzitaka taasisi za umma na zile binafsi kushirikiana vyema na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali.

Asema kuwa takwimu zina umuhimu mkubwa katika maendeleo ya nchi pamoja na wananchi wake na zimekuwa zikisaidia kwa kiasi kikubwa katika kufanya maamuzi, kuwahudumia wananchi pamoja na kuzisaidia Wizara katika kutekeleza mipango yake.

Semina hiyo ilikuja na maazimio ambayo yalisomwa mbele ya washiriki wote kufuatia mada tano silizowasilishwa na wasilishaji mbali mbali kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali zenye maudhui tofauti ikiwemo mada ya Muhtasari wa majukumu ya Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali katika upatikanaji wa takwimu na matumizi yake.
 
Mada nyengine ilikuwa ni Umuhimu wa takwimu, hatua za uzalishaji na matumizi yake, Takwimu za sekta ya kilimo, Takwimu za sekta ya viwanda na Takwimu za sekta ya huduma.


Post a Comment

 
Top