0


Burundi ilundwa kama ufalme ulioongozwa na Watutsi waliotawala Wahutu. Lakini kabla ya ukoloni mipaka kati ya makundi hayo haikuwa imara mno; Wahutu matajiri katika utumishi wa mwami waliweza kupanda ngazi na kuwa Watutsi na pia Watutsi maskini waliweza kushuka ngazi na kuhesabiwa kati ya Wahutu, hasa baada ya kuoa au kuolewa na mtu wa upande mwingine. Uhusiano wa makundi hayo ulifanana zaidi na ule wa matabaka si wa makabila tofauti, pia kwa sababu lugha ilikuwa moja kwa wote.
Utawala wa kikoloni uliimarisha mipaka kati ya makundi hayo mawili maana kila mtu aliandikishwa na kupangwa katika moja kati ya makundi hayo. Pia Wabelgiji walipendelea Watutsi na kuangalia wapate nafasi zote za uchifu ambako walipaswa kutoa kibali. Kuhamia katika kundi lingine kulikwisha. Uhusiano kati ya makundi ulianza kufanana zaidi na ukabila.
Mwishoni mwa ukoloni Wabelgiji walibadilisha msimamo na kupendelea Wahutu.















Katika hali hiyo Burundi ilikaribia uhuru. Vyama vya siasa viliundwa vilivyofuata ugawaji wa kimbari kati ya Watutsi na Wahutu. Mapigano ya kwanza kati ya Wahutu na Watutsi yalitokea mwaka 1959 kabla ya uhuru yakakomeshwa na Wabelgiji.
Baada ya uhuru katika Burundi, kinyume na Rwanda, utawala ulibaki upande wa Watutsi kwa sababu jeshi lilikuwa mikononi mwao. Vipindi vya mashambulio kati ya vikundi vilifuata.



Mwaka 1972 malaki ya Wahutu waliuawa na jeshi la Kitutsi waliolenga hasa Wahutu wenye elimu.
Mwaka 1993 uongozi wa Kitutsi ulikubali tena uchaguzi huru ambako Mhutu Melchior Ndadaye alichaguliwa kuwa rais. Alipouawa na wanajeshi Watutsi malaki ya Watutsi waliuawa na Wahutu wakali.
Kipindi kilichofuata kilikuwa cha Vita ya wenyewe kwa wenyewe katika sehemu mbalimbali za nchi.
Tangu mwaka 1995 Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa zilijitahidi kujenga mapatano kati ya vikundi. Marais na wanasiasa walioshiriki katika jitihada hizo walikuwa pamoja na Julius Nyerere, Boutros Boutros-Ghali, Nelson Mandela, Thabo Mbeki na rais wa Marekani Bill Clinton.
Mapatano yalifikiwa na kusainiwa mwaka 2000 na washiriki karibu wote huko Arusha. Majadiliano yaliendelea hadi mwaka 2003 hatimaye vita ilisimamishwa. Mapatano yaliyofikiwa yanasema ya kwamba Watutsi pamoja na Watwa, ambao ni asilimia 15 za wananchi, watakuwa na asilimia 40 ya nafasi kwenye bunge na ya kwamba jeshini kila upande utashika asilimia 50 za nafasi. Pia kwenye senati ya bunge kila upande utakuwa na asilimia 50. [8]
Rais atachaguliwa na wananchi wote lakini mapatano yalisema rais wa kwanza atachaguliwa na bunge.
Hali ya kisiasa hivi sasa sionzuri lakini Hii Ndiyo Orodha ya Maraisi wa Nchi ya Burundi..

28 Novemba 1966 – 1 Novemba 1976     Michel Micombero

 


2 Novemba 1976 – 3 Septemba 1987 Jean-Baptiste Bagaza




3 Septemba 1987 – 10 Julai 1993 Nchi ilikuwa Chini ya Jeshi

 

3 Septemba 1987 – 10 Julai 1993  Pierre Buyoya



 

10 Julai 1993 – 21 Oktoba 1993  Melchior Ndadaye







21 Oktoba 1993 – 27 Oktoba 1993  François Ngeze 


























5 Februari 1994 – 6 Aprili 1994 Cyprien Ntaryamira

27 Oktoba 1993 – 5 Februari 1994  Sylvie Kinigi (mtendaji tu/acting President)

 

  6 Aprili 1994 – 25 Julai 1996   Sylvestre Ntibantunganya

 

 

 25 Julai 1996 – 30 Aprili 2003         Pierre Buyoya (mara ya pili)

 

30 Aprili 2003 – 26 Agosti 2005  Domitien Ndayizeye

 

26 Agosti 2005 – leo     Pierre   Nkurunziza

Post a Comment

 
Top