0



Ligi daraja na tatu limefungua pazia februari 24 katika kituo cha Liwale kwa mchezo kati ya timu ya Sido fc dhidi ya Hawili fc mpaka dakika 90 matokeo yalikuwa sare ya goli 1-1  mchezo uliopigwa katika uwanja wa halmashauri ya wilaya ya Liwale mkoani Lindi.

Katika kituo cha Liwale kilikuwa na jumla ya timu mbili zinazoshiriki  ambazo zote zilitokea hapa hapa wilayani ambazo ni Sido fc na Hawili fc hivyo kukosa ushindani mkubwa.

Timu ya Hawili fc ilikuwa ya kwanza kupata goli lililofungwa na Rehmani Mtipa namo dakika ya 14 goli hilo lilidumu mpaka mapumziko ya dakika 45 kipindi cha kwanza.

Katika kipindi cha pili Timu ya Sido fc ilibadilisha mchezo huku ikicheza kutaka kusawazisha goli lakini walizidiwa mbinu za kimchezo katika dakika ya 75 mchezaji wa Hawili fc,Rashidi Gumbo alijifunga mwenyewe kwa mpiga kichwa katika harakati ya kutaka kuokoa baada ya kupiga pasi ndefu Haikosi Mpwate kuelekeza kwenye lango la Hawili fc na kupelekea kupigwa mikwaju ya penaiti ili kumpata mshindi mmoja.

Hatua ya upigaji wa penaiti ilianza kwa upande timu ya Sido fc iliweza kupata goli 1 ikikosa penaiti 3 moja akificha mlinzi wa Hawili fc Masoud huku timu ya Hawili ilipiga mikwaju mitatu na kuweza kutisa nyavu mara tatu.

Kocha wa timu ya akizungumza na Liwale Blog,Mohamedi Hema alikili kufungwa katika mchezo huo pia aliweza kuzungumzia juu ya waamuzi wa mchezo huo alisema waamuzi walichezesha vizuri nae kocha wa Hawili fc,Hasani Malapo alisema mchezo ulikuwa mzuri kwa pande zote ushindi walioupata ulitokana na maandalizi mazuri japo ligi haikuwa na changamoto sana kutokana na kituo kushiriki timu mbili.

Post a Comment

 
Top