Bilionea wakitanzania na mmiliki wa makampuni ya IPP Bwana Reginald Mengi aliwahi kusema kupitia ukurasa wake wa twitter kuwa, “Mwogope mtu anayesema yupo na wewe ukigeuka nyuma hayupo. Huyo ni mnafiki.”
Hayo ni maneno magumu lakini yana kitu kikubwa cha kujifunza ndani
yake. Kuna jambo nataka tujifunze kwa kupitia ujumbe huo mfupi hasa
wakati kama huu tunapoelekea kumaliza mwaka huu 2016 na kuutafuta mwaka
2017. Jambo hili ninalotaka ujifunze na kulizingatia ni juu ya “kufanya
uchaguzi makini wa kuchagua marafiki au watu wa kushirikiana nao katika
malengo na mipango yako uliojiwekea hadi hivi sasa kwa ajili ya mwaka
ujao.”
Usikubali kutembea na kila mtu kwenye njia zako, bali amua kuweka
uchaguzi sahihi wa kujua ni nani wa kwenda nae ili uweze kufanikisha
malengo na ndoto yako uliyonayo. Kusema nitafanya jambo fulani na kila
mtu, huku ni wazi si kila mtu ana uwezo wa kubebana na jambo unalotaka
kufanya au kukupa nafasi ya kusogea mbele na kupiga hatua, yawezekana
umeamua kuwa nae kwa sababu ya huruma, au uliwahi kusoma nae au ni
rafiki yako wa zamani nk. Hapana. Hatuendi na kila mtu kanaani kwa
sababu wote ni wa Israel ila ni wale walio na moyo wa utayari wa kwenda
huko, na wale tu wenye nafasi ya kukubali magumu ya njiani kukubali
kutembea pamoja nawe.
Wakati mwingine tumejikuta tunaingia katika maumivu makubwa kwa
sababu ya kujaribu kuweka matumaini yetu kwa watu fulani pasipo kujua
watu hao wanatuwazia nini ndani yao. Usiweke matumaini yako
(expectations) kwa 100% kwa mtu ambaye hujampima na kumjua ana mwelekeo
gani binafsi kwenye kuifata na kuishi ndoto yake mwenyewe na zaidi sana
kwako wewe ambae umeamua kumshirikisha mambo yako uliyonayo. Usimtegemee
mwanadamu kwa 100% bali amua kuweka uamuzi chanya wa kujisimamia wewe
mwenyewe kama hatua za kwanza za kujijengea msingi mzuri wa kule
unapoelekea, kisha kaa chini na utafakari kwa makini ni yupi unayeweza
kwenda nae ili kuleta matokeo chanya kwenye maisha yako.
FANYA ZOEZI HILI:
1: Chukua kipande cha karatasi au notebook au diary yako ya mwaka 2017.
2: Orodhesha majina ya watu wa 5 au 10 unaotaka wakusaidie katika kutimiza malengo na ndoto yako kwa mwaka 2017.
3: Katika orodha ya majina yako amua kuchagua mtu
mmoja au wawili tu utakaowashirikisha mara kwa mara kila kitu
unachoendelea kufanya au unachofanya ili waweze kukuongoza na kukupa
msaada juu ya unachofanya. Kumbuka amua kuwa na mtu mwaminifu na
unayemwona anafaa kwa kile unacholenga wewe katika kukifanikisha.
Usijaribu kuwa na kila mtu.
4: Watafute wahusika kwa kuwasiliana nao haraka. Usiogope. Jiamini.
KWA USHAURI ZAIDI:
Kwa ushauri zaidi ya namna ya kufikia malengo yako ya 2017 na
hatimaye kuweza kutimiza ndoto yako uliyonayo, kuwa huru kuwasiliana
nami kupitia mawasiliano yangu hapo chini ya website, nami nitakupa
msaada wa bure kabisa. Usikubali kutembea mwenyewe bali kuwa karibu na
mtu mwaminifu aliye na utayari wa kukusaidia na anayeweza kukuongoza
(coaching) hasa katika kufikia ndoto yako.
JIAMINI NA AMINI UNAWEZA. ISHI NDOTO YAKO.
Simu: 0767 500994 (WhatSapp Group – IshiNdotoYako)
Barua pepe: info@ishindotoyako.com
Ni Mimi mmiliki na mwanzilishi wa tovuti namba moja ya mafunzo ya
kuhamasisha kwa lugha mama ya kiswahili, inayosomwa na watu wengi
wanaotumia lugha hii ya kiswahili duniani. Nakupenda sana na usiache
kutembelea mtandao huu mwaka ujao kwa kusudi la kujifunza zaidi na zaidi
ili kupiga hatua ya kufikia ndoto yako. Nikutakie mwaka 2017 ulio na
ushindi na mafanikio kiroho na kiuchumi zaidi.
Post a Comment