0

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Musoma vijijini mkoani Mara limeagizwa kuchukua hatua kali kwa uongozi wa kituo cha afya cha Murangi katika halmashauri hiyo, baada ya kudaiwa kutumia gari la wagonjwa kufanya biashara ya kubeba abaria na kusababisha gari hilo la kisasa kuharibika katika kipindi kifupi baada ya kununuliwa.

Waziri wa Nishati na madini ambaye pia ni Mbunge wa Musoma vijijini Mh Prof Sospeter Muhongo,ametoa agizo hilo baada ya kukabidhi misaada ya vitu mbalimbali zikiwemo baiskeli nne za kubebea wagonjwa na vitanda kumi  kwa ajili ya wagonjwa wanaolazwa katika kituo hicho kinachotumika hivi sasa kama hospitali ya halmashauri ya wilaya na kuelezwa kuhusu kuharibika kwa gari hilo.
Naye mkuu wa wilaya ya Musoma Dk Vicent Naano, akizungumza baada ya Mbunge huyo wa Musoma vijijini kutoa agizo hilo,amesema serikali itachukua hatua kali kwa watu waliosababisha kuharibika kwa gari hilo la kisasa la wagonjwa katika kituo hicho.

Post a Comment

 
Top