0
MFANYABIASHARA wa ndizi amefariki dunia baada ya kupigwa na radi na wengine wanne kujeruhiwa, wakati mvua kubwa ilioambatana na radi ikinyesha katika eneo la Stendi kuu mjini Tukuyu Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Dk Marco Mbata amemtaja Mfanyabiashara huyo kuwa ni Freman Swai mkazi wa Mkoani Arusha, ambaye anadaiwa alikuwa Tukuyu kwaajili ya kununua ndizi,na kwamba amefariki wakati akipatiwa matibabu kwenye hospitali ya Makandanda baada ya kupigwa na radi ambayo pia imechana chana mti mbichi uliokuwa karibu na kibanda ambacho marehemu alikuwa amejikinga asilowe na mvua .
Amewataja majeruhi kuwa ni,Oliva Ipyaja Anna Jelicho Juliana Francis Stella Nzite, wote wakazi wa Tukuyu, ambao wametibiwa na kuruhusiwa na kwamba mwili wa mfanyabiashara huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya makandana
Aidha Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Julius Challya amesema tayari ndugu wa mfanyabiashara huyo wameshafahamika, lakini pia amewataka wananchi kuwa makini matumizi ya vifaa ambavyo ni hatarishi vinavyoweza kuruhusu radi kupiga hususani nyakati za mvua, ili kuepuka vifo visivyo vya lazima.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top