Mkuu
wa wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga akiwa na kamati ya ulinzi na usalama
baada ya tuhuma hizo za barabara hiyo kujengea mitaro kwa kutumia tope
imemlazimu kutembelea mradi huo na kubaini ujenzi huo , ambapo alikuta
kmtaro hiyo imejengwa kwa kutumia udongo huku ikichapiwa na sementi.
Kiswaga
akalazimika kutumia jembe wakati wa ukaguzi huo kwa ajili ya
kujiridhisha ukweli huo, ambapo pia yalitokea mabishano makubwa baina ya
Mkuu huyo wa wilaya, wahandisi wa halmshauri, mhandisi mashauri kutoka
NOLPLAN pamoja na Mkandarasi JASCO CO.LTD juu ya ujenzi huo kwa
wanapunguza gharama.
Katika
mabishano hayo yaliyodumu takribani dakika 15 wataalamu hao ambao
walikuwa wakimbishia mkuu huyo wa wilaya kuwa kilichojengwa siyo mtaro
bali ni mwanzo wa mtaro (foundation), huku wakikiri kuwa walitumia tope
kujengea.
Kutokana
na hali hiyo Kiswaga aliamuru mitaro hiyo iliyojegwa kwa tope
kubomolewa mara moja, huku akiagiza kuwekwa rokapu Mkandarasi kutoka
JASCO Co.Ltd, Mhandishi Mshauri NOLPLAN pamoja na Mhandisi msaidizi wa
halmashauri Brayson Fadhili.
Post a Comment