0


Mabingwa mara tatu wa kombea la Mapinduzi Simba fc ya Dar es Salam imeanza vema mashindano ya mapinduzi Cup  yanayoendelea Visiwani Zanzibar baada ya kuwafunga goli 2-1 Timu ya Taifa Jangombe (Maarufu kama wakombozi wa Ng’ambo) mchezo ambao umepigwa katika Uwanja wa Amani.

 Mchezo huo umepigwa majira ya saa 2:30 za Usiku  ambapo Simba walipata goli lao la kwanza kupitia kwa kiungo wake Mzamiru Yasini katika dakika ya 28 huku Juma Luzio anaekipiga Simba kwa mkopo akitokea Zesco United ya Zambia akifunga bao la 2 kwa Simba  katika dakika ya 41, lakini Timu ya Taifa ya Jang’ombe  walipata bao la kufutia machozi baada beki wa Simba Novatus Lufunga kujifunga katika dakika ya 76 kufuatia mpira wa kona kumgonga na kuingia wavuni

Mchezo huo ni wa kwanza kwa Simba lakini ni wa Pili kwa Timu ya Taifa Jang’ombe baada ya mchezo wa kwanza kushinda kwa bao 1 kwa sifuri dhidi ya Jang’ombe Boys mchezo ambao umepigwa siku ya ufunguzi  wa mashindano hayo desember 30 katika uwanja wa amani.

Awali majira ya saa 10:30 hapo jana, kulikuwa na mchezo wa kwanza ambapo mabingwa watetezi URA kutoka Nchini Uganda walishuka Dimbani kucheza na KVZ  na URA kufanikiwa kwa kupata ushindi wa mabao mawili kwa 0

Kutokana na matokeo hayo katika msimamo wa kundi A,URA yuko kileleni akiwa point 3 na magoli 2,huku Simba akiwa nafasi ya pili, pointi zake 3  na magoli mawili na  nafasi ya tatu inashikiliwa na Taifa Jang’ombe akiwa na point 3 na goli 2 huku nafasi ya mwisho ikibakia kwa Jang’ombe Boys ambao wamecheza mchezo 1 na kupoteza.

Ligi hiyo ya mapinduzi cup itaendelea hii leo kwa kupigwa michezo miwili wakati mchezo wa mapema utakuwepo kati ya Zimamoto na Azam huku mchezo wa majira ya saa mbili za Usiku ukiwakutanisha Dar  es Salaam Young African dhidi ya Jamhuri kutokea Visiwani Pemba.


Post a Comment

 
Top