0

MGANGA mkuu wa Hospitali ya Wilaya Geita Rafhael Mhana pamoja na Mganga Mfawidhi wa kituo cha Afya kata ya katoro Peter Janga wamezomewa mbele ya Mkuu wa Wilaya hiyo Heruman Kapufi baada ya kutoa taarifa za uwongo kuwa wananchi wote wanaochangi mfuko wa NHIF wanapata dawa zote pale wanapokwenda kupata uduma ya Afya.
screen-shot-2017-01-05-at-2-41-57-pm
Hali hiyo imejitokeza jana majira ya saa kumi na moja jioni kwenye mkutano wa adhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi katoro uliokuwa na lengo la kuimiza maendeleo na kusikiliza kero za wananchi waanza kueleza.
Mara baada ya waganga hao kumaliza kueleza juu ya upatikanaji wa dawa ndani ya kituo chao hali ilibadilika na kuwa hivi huku wakimtaka mkuu huyo kuwatumbua kwa kumdanganya.
Mkuu huyo wa Wilaya alilazimika kuokoa jahazi kwa kuwatuliza wananchi hao walionekana kuwa jaziba kubwa juu ya uwongo wanaoueleza mbele ya kiongozi huyo na hapa wakanza kueleza kero zao wanapokwenda kupata uduma katika kituo hicho cha afya.
Walipomalizaa kutoa kero zao nyingi zilizoonekana kuwa na tija kubwa na mkuu huyo na hapa akatoa neno juu ya wauguzi wazembe kwenye kwenye Wilaya yake.
Mkuu huyo anaendelea na ziara yake kwenye kata 50 zilizoko ndani ya Wilaya yake lengo likiwa ni kuimiza kuchangia maendeleo pamoja na kusikiliza kero za wananchi.

Post a Comment

 
Top