0
Tokeo la picha la korosho
Jeshi la polisi mkoani Mtwara linawashikilia watu sita wakiwa na magari mawili ya mzigo ambao walijaribu kusafirisha tani 29 za korosho kupitia bandari ya Mtwara zinazosadikika kuwa zimenunuliwa nje ya mfumo wa stakabadhi gharani maarufu kama Kangomba.
Watu hao wamekamatwa bandarini jana majira ya saa mbili usiku wakiwa na vielelezo feki.
Jana majira ya saa mbili usiku dereva Bakari Seleman akiendesha lori namba T 870 AHS likiwa limebeba magunia 150 pamoja na dereva Emanuel Luckas akiendesha lori namba T 529 AJR likiwa limebeba magunia 220 ya korosho,wakiwa na wafanyabiashara wawili wenye asili ya Asia pamoja na wasaidizi wao,waliwasili geti namba tatu la bandari ya Mtwara kwa ajili ya kupitisha mzigo huo ili uweze kusafirishwa.
Wafanyabiashara hao walikuwa na vielelezo bandia vya mzigo huo hali ambayo ikawafanya kutiliwa mashaka na askari wa mamlaka ya bandarini.
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mtwara ambae ni mkuu wa mkoa huo Halima Dendego anasema haijalishi msimu wa korosho unaelekea mwisho zoezi la kupambana na udhibiti wa kangomba bado unaendelea.

Post a Comment

 
Top