0

MAKATIBU na Washika fedha Wa mfuko wa maendeleo ya majimbo Kisiwani Pemba wametakiwa kusimamia vizuri fedha zinazotolewa na Serikali kupitia mfuko huo katika kuhakikisha  miradi wanayosimamia inatekelezeka.

Ushauri huo umetolewa na Naibu waziri Ofisi  ya Makamo wa pili wa rais Mhe. Mihayo Juma Nhunga alipokuwa akifunguwa mafunzo ya siku moja kwa makatibu, wakurugenzi na washika fedha  wa mfuko wa maendeleo ya  jimbo huko katika ukumbi wa Tassaf.
 waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe Mihayo Juma  akifungua mafunzo ya siku moja watendaji wakuu wa Mfuko wa Jimbo Kisiwani Pemba.



Amesema katika awamu iliyopita  fedha hizo hazikutumika vizuri  katika utekelezaji wa miradi mbali mbali ndani ya majimbo  hali ambayo wasimamizi walishindwa  kuwasilisha  ripoti ya matumizi ya fedha za miradi hiyo.

Nae Mkurugenzi  Uratibu wa Ofisi ya Makamo wa pili wa Rais  Nd,Khalid Bakar Hamad na Afisa Mdhamini wa Ofisi hiyo Ali Salim Matta wamesema fedha hizo  zinazotolewa  na Serikali  sio sadaka na badala yake  zitumike katika kuwaletea wanachi maendeleo majimboni.


Post a Comment

 
Top