0


Na mwanishi wetu Zanzibar                                                         

AFISA Mdhamini Wizara ya Afya Pemba Bakar Ali Bakar amebaini kuwepo na  upotevu wa mashuka 36 na mito 20 katika Hospitali ya Wete  na kuuagiza uongozi wa hospitali hiyo kuhakikisha vifaa hivyo vinapatikana ndani ya kipindi cha wiki mbili.


Amesema upotevu wa mashuka na mito hiyo ameubaini kufuatia ziara yake ya kukagua  utoaji wa huduma kwa wagonjwa katika hospitali hiyo ambapo alipokea malalamiko kutoka kwa wagonjwa juu ya ubovu wa mashuka katika vitanda vya wodi ya watoto.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana Ofisini kwake ,Bakar amesema  ziara hiyo aliyoifanya akiwa ameambatana na maafisa wa Wizara hiyo Pemba , alishuhudia  vitanda vikiwa na mashuka machakavu.

Ameeleza kwamba hali hiyo ilimfanya ahoji sababu zinazowafanya kuendelea kutumia mashuka yaliyochakaa  licha ya Serikali kuandaa mazingira mazuri ya upatikanaji huduma bora kwa wagonjwa ikiwemo suala la malazi.

Post a Comment

 
Top