0


Na Mwandishi wetu zanzibar

Ofisi ya Mufti Zanzibar  imeliomba Jeshi la Polisi Zanzibar kumchukulia hatua za kisheria kijana Abdalla Saleh anaedaiwa  kutoa matamshi ya kumkashifu  Mtume Muhammad (s.a.w).

Mufti Mkuu  wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kaabi



Akitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari ofisini kwake Mazizini Mjini Unguja Mufti Mkuu  wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kaabi amesema matamshi yaliyotolewa na kijana huyo yanaweza kuvuruga amani ya nchi na kuharibu uhusiano wa Zanzibar kimataifa.
Pamoja na hayo, mufti mkuu ametoa onyo kwa waumini wa dini hiyo kutokutowa  maneno yenye kuikashifu imani yao.
Aidha amewasihi waislamu wote kuwa watulivu na kusubiri vyombo vya kisheria kumchukulia hatua kijana huyo

Post a Comment

 
Top