NB-Picha haihusiani na habari hapa chini
Watu watano wamefariki dunia na sita kujeruhiwa baada ya kuangukiwa na mwamba wa mawe katika shimo la mgodi wa zamani wa Resolute Nzega mkoani Tabora.
Inaelezwa kuwa tukio hilo limetokea
baada ya kundi la wachimbaji wadogo wa mgodi wa Umoja kuvamia eneo hilo
ambalo limepigwa marufuku na serikali.
Akizungumzia tukio hilo Mkuu wa wilaya
ya Nzega Godfrey Ngupulla amesema eneo hilo limezuiwa kuchimbwa kutokana
na hatari iliyopo lakini baadhi ya wachimbaji wamekuwa wakiingia kwa
kificho kuchimba.
Amewataja walipoteza maisha kuwa ni
Joseph Mpenda,mkazi wa Shinyanga,Mohamed Mohamed,mkazi wa Singida,Manona
Nyombi,mkazi wa Bariadi na Modesta Leonard,mkazi wa Nzega.
Waliojeruhiwa ni Kang'wa Mayenga,mkazi
wa Bariadi,Agnes Anthony,mkazi wa Chato,Deus Alponce,mkazi wa Igunga na
aliyefahamika kwa jina moja la Mapunda mkazi wa Chato.
Post a Comment