Zaidi ya wanafunzi
laki tano waliofanya mtihani wa Kiwango cha shule ya upili, nchini Kenya
wamepokea matokeo yao leo kwa manung'uniko.
Waziri wa Elimu,
nchini humo, Fred Matiangi aliyatangaza matokeo hayo mjini Mombasa
kinyume na ilivyokuwa awali ambapo mji wa Nairobi ulitumika kufanya
shughuli hiyo.
Matokeo hayo yameonyesha kupungua kwa alama bora
ikilinganishwa na miaka ya awali. Ni asilimia 15 tu ya wanafuzi wamefuzu
kujiunga na elimu ya chuo kikuu kwa moja.
Aidha wasichana
walifanya bora katika orodha ya wanafuzi 20 bora nchini humo. Kumi na
sita kati yao walikuwa ni wasichana huku wavulana wakiwa ni wanne pekee.
"Shule nyingi zilizokuwa zinaandikisha A nyingi, zimepata mbili pekee," alisema.
Bwana
Matiangi aliyebandikwa jina Magufuli, baada ya Rais wa Tanzania John
Magufuli, alisema kupungua kwa matokeo bora ilikuwa ni mafaniko ya
kuziba nyufa za wizi wa mtihani.
Hata hivyo, hakuna kisa chochote cha udanganyifu kilichoripotiwa.
Wakati
huo huo, Rais Uhuru Kenyatta ametoa agizo la kuondolewa kwa nambari ya
mtihani kuwatambulisha wanafunzi na kubadilishwa na nambari ya siri.
Taifa
hilo lilikumbwa na wimbi la kuteketezwa kwa mabweni na wanafunzi baad
aya sheria kali za kuzuia wizi wa mtihani kufanikishwa na waziri huyo.
Post a Comment