0


Waziri  wa elimu na mafunzo ya  amali zanzibar mhe Riziki Pembe Juma  amewataka  walimu wakuu kuwahamasisha wanafunzi wao kupenda kusoma masomo ya sayansi  na  kuwafanya  waondoe  dhana  ya kwamba masomo hayo ni magumu. .
 waziri wa elimu zanzibar Riziki Pembe Juma

Ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa nne wa Jumuiya ya walimu wakuu Zanzibar (JUWASEZA) ambapo  amesema  sio  jambo la busara kwa mwanafunzi kuchagua masomo wakati akiwa skuli za sekondari , na kufahamisha kwamba kitendo hicho kimechangia kushuka kiwango cha ufaulu wa wanafunzi katika skuli za Unguja na Pemba.


Sambamba na hilo amewataka walimu wakuu kuacha kujihusisha na masuala ya siasa sehemu za kazi kwani wanaweza kusababisha kuzorotesha ufanisi wa kazi ya kuwaandaa vijana kuweza kukabiliana na changamoto za utandawazi.
Mapema Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman amepogeza hatua zinazochukuliwa na Jumuiya ya Walimu Wakuu Wa Sekondari Zanzibar katika kuzipatia ufumbuzi  changamoto za Elimu na kuahidi kwamba Serekali ya Mkoa itaendelea kushirikiana na Jumuiya hiyo. 
       
Nae Katibu mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar  bi Khadija Bakar Juma amewataka Walimu Wakuu kuwa chanzo cha Maadili, Uwajibikaji na ufundishaji ili kuongeza idadi ya ufaulu wa Wananfunzi

Post a Comment

 
Top