0



















Wanaccm nchini wamewatakiwa  kujiweka tayari katika kuandikisha daftari la kudumu la wapiga kura katika Majimbo mbali mbali Zanzibar  muda utakapowadia.
 Akizungumza katika ziara ya kuhimiza uhai wa chama mkoa wa kaskazini Unguja katibu wa kamati maalum ya nec wa idara ya itikadi na uenezi mh: Waride Bakari Jabu pia amewataka viongozi wa Wilaya kuweka takwimu sahihi ya orodha ya wanachama katika daftari la wanachama wa Chama Cha Mapinduzi.
Sambamba na hayo mh: Bi Waride amesisitiza haja kwa wanachama kuendeleza upendo, umoja na mshikamano wa dhati  miongoni mwao na kuwa makini zaidi katika kufuatilia minendo ya ndani na nje ya chama.

Aidha amewataka wanaccm kushirikiana baina ya wanachama katika ngazi ya Tawi ili  kupanga mikakati itakayoleta ushindi mkubwa  katika  uchaguzi wa mwaka 2020.
        Pia amewataka wanachama wa Matawi husika waishi kwa furaha kwa ushindi wa kishindo wa katika nafasi za  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Rais wa  Zanzibar, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani. 
Katika hatua nyengine mh: Waride amewataka wanaCCM wajiandae na Uchaguzi wa kutafuta uongozi wa Chama 2017 na kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbali mbali ili kuwapata viongozi walio bora.

Halikadhalika amewasihi wanachama kujiepusha na vitendo vya rushwa na udanganyifu katika kutafuta uongozi ndani ya chama hicho.
Aidha amewakumbusha viongozi kuwaeleza wananchi juu ya mambo yote ambayo yametekelezwa kupitia Serikali pamoja na viongozi wa Majimbo kama Wabunge, wawakilishi pamoja na Madiwani.
Nao wanachama hao wameuomba uongozi CCM kutoka afisi Kuu kufanya ziara za mara kwa mara ili wananchi wawe na hamasa na viongozi wao wa Chama.

Post a Comment

 
Top