0


        Jeshi la polisi mkoa wa mjini magharibi limemkamata kijana aliedaiwa kumchoma moto mpenzi wake na kumsababishia majeraha makubwa mwilini.
Add caption

Tukio la kukamatwa kwa kijana huyo linajiri siku moja baada ya waziri mwenye dhamana ya maswala ya wanawake mh: moudline castiko kuomba vyombo vyenye dhamani kulifanyia uchunguzi suala hilo.


Hapo jana waziri wa kazi,uwezeshaji,wazee,wanawake na watoto Mh:Modelin   Castico alimtembelea ndugu Samira Abbas Ameir alieunguzwa na moto na mpenzi wake katika  hospital  ya  kivunge  ya  koteji makunduchi  kusini  Unguja.
Akiwa hospitalini Mh: Castico amesema Serikali  ya mapinduzi Zanzibar haitolifumbia  macho  tukio  la kuchomwa moto kwa binti huyo na  sheria  lazma  ichukue  mkondo wake.
Aidha  amevitaka vyombo  husika  vya  ulinzi  na  usalama, wanasheria na  watu  wote  wanaotetea  haki  za  wanawake  kushirikiana  ili  kupunguza  vitendo  hivyo.

Kwa  upande  wa  majeruhiwa  huyo mwenye umri  wa  miaka  26  ambae   ni  mkaazi  wa  Paje  kusini  Unguja  amesema kisa  cha  tukio  hilo  ni  baada ya kumtamkia  mpenzi wake huyo kua  kamchoka  na  anataka  kurudi   kwao.

Post a Comment

 
Top