0


Mkuu wa Wilaya ya Wete Rashid  Khadidi Rashid amewataka madaktari wa Wilaya ya hiyo kuendelea kutoa huduma bora kwa mama  wajawazito na mtoto ili kujiongezea sifa.

     Mkuu wa Wilaya ya Wete Kisiwani Pemba Rashid  Khadidi   Rashid(kulia)



       
   Amesema hatua ya  hospitali ya Wete kupata ushindi wa kwanza katika utowaji wa huduma ya mama wajawazito na watoto ni ya kupongezwa kwani ni miongoni mwa mikakati ya serikali ya kupambana na vifo vya mama na watoto.

        Mkuu huyo wa wilaya  ametoa wito huo katika ukumbi wa Benjameni Mkapa Wete kwenye sherehe za kupongezana kwa madaktari  walioshiriki katika utowaji wa huduma hiyo  kwa kupata washindi wa kwanza kwa hospitali zilizotekeleza mradi huo Unguja na Pemba.

       Aidha amewataka madaktari hao kua mfano bora katika utoaji wa huduma za afya kwa jamii ikiwa ni pamoja na kutumia lugha nzuri wakati wa kuwahudumia  wagonjwa ili wafurahie huduma zao.

      Nae  daktari Mkuu kisiwani Pemba Mbwana Shoka  amesema pamoja na uchache wa madaktari lakini wameweza kufanikiwa kutoa huduma ya mama na mtoto na kupata ushindi wa kwanza kati ya  hospitali nane za Zanzibar zilizoshiki katika

Post a Comment

 
Top