Waziri wa
nchi ya ofisi ya makamo
wa pili wa
Rais Zanzibar Mohammed Aboud ametoa
tamko rasmi la
kuanza kwa sherehe
za mapinduzi matukufu
ya 53 ya zanzibar .
Akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake
vuga mjin Zanzibar, Mhe. Aboud amesema
shamrashamra hizo zitaanzia
kesho ambapo kutafanyika shughuli
ya usafi nchini ikifuatiwa na Januari Mosi ambapo Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein
atawaongoza wananchi katika mazoezi ya
viungo kutembea.
Miradi
mbali mbali itazinduliwa kuelekea kilele cha sherehe za Mapinduzi Zanzibar
Januari 12 mwakani, ikiwemo barabara ya Kwerekwe - Fuoni, sacoss ya meli nne
wilaya ya magharib, kituo cha
zimamoto kilichopo uanja wa ndege na pia
kuwekwa jiwe la
msingi katika nyumba
za zssf.
Post a Comment