Benki
ya Kimataifa ya Exim ya Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China imeahidi
kuendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kusaidia
Maendeleo ya Wananchi wake kupitia miradi tofauti inayoanzishwa.
makamo wa pili wa raisi serikali ya mapinduzi Zanzibar balozi Seifu ali iddi
Bwana Sun Ping amesema Taasisi hiyo ya Fedha ya China imeridhika na hatua kubwa ya maendeleo iliyofikiwa na Zanzibar katika kuimarisha uchumi wake kiasi kwamba Benki hiyo itaangalia namna za kusaidia nguvu katika kuona miradi inayoanzishwa inatekelezwa.
Makamu
wa Rais wa Benki hiyo ya Exim alimueleza Balozi Seif na Ujumbe wake kwamba
Tanzania ndio nchi pekee iliyopewa kipaumbele na benki hiyo katika
kupatiwa mikopo na misaada ikilinganishwa na Nchi nyengine Barani
Afrika.
Akitoa
shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
aliipongeza Benki hiyo ya Exim kwa ukarimu wake wa kuunga mkono miradi ya
Maendeleo inatotekelezwa Zanzibar kwa njia ya misaada na hata mikopo.
Balozi
Seif amesema yapo mafanikio makubwa yaliyopatikana miongoni mwa Wanachi
waliowengi Zanzibar kufuatia kuibuka kwa miradi kadhaa ya Kiuchumi na
maendeleo iliyopata msukumo kupitia Benki hiyo ya Kimataifa ya Exim.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.