Na mwandishi
wetu Zanziab
Raisi wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amezipongeza
Serikali za Oman na ile ya Cuba kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika
kuendeleza miradi ya maendeleo sambamba na kuimarisha uhusiano na ushirikiano
wa kihistoria uliopo kati ya Zanzibar na nchi hizo.
Akizungumza
kwa nyakati tofauti wakati alipokutana na Mabalozi wa nchi hizo Ikulu mjini
Zanzibar hapo jana, Dk. Shein amezipongeza nchi hizo kutokana na ushirikiano
wanaoutoa na kuutaja kuwa chachu katika kuimarisha juhudi za Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika kujileta maendeleo.
Awali akizungumza
na Balozi wa Cuba katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bwana Jorge Luis Lopez Tormo ambae kwa sasa amemaliza muda wake wa kazi hapa nchini, Dk.
Shein ameeleza kuwa mbali na madaktari kutoka katika nchi hiyo ambao wamekuwa
wakija nchini kusaidia katika sekta ya afya tangu 1964, Cuba imekuza uhusiano
wake kupitia sekta hiyo kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiwemo
kuanzisha chuo cha Udaktari ambacho tayari kimeshaanza kuzalisha matunda kwa
kutoa Madaktari Wazalendo.
Aidha,
amesema kuwa mbali ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya afya kwa nchi hizo
mbili ameelezea azma ya kuanzisha ushirikiano katika sekta ya utalii kutokana
na Cuba kupiga hatua kubwa katika sekta hiyo.
Nae Balozi
Jorge Luis Lopez Tormo alimuhakikikishia Dk. Shein kuwa Cuba itaendeleza miradi
yote ya maendeleo inayoishirikisha nchi yake huku akiweka wazi kuwa nchi yake
itafarajika kwa kuwepo ushirikiano katika sekta ya utalii.
Amesema kuwa
kwa mwaka huu pekee, Cuba imeweza
kupokea watalii wapatao milioni tatu na nusu na kukiri kuwa mfanano wa miji
mikongwe ya Zanzibar na Havana unaweza kuwa chachu katika kukuza utalii kwa
pande zote mbili.
Katika hatua
nyengine Dk. Shein alifanya mazungumzo na Balozi Mdogo mpya wa Oman, Ahmed Bin
Humoud Al Habsi, ambapo alitumia fursa hiyo kuipongeza Oman kwa kuendelea
kuiunga mkono Zanzibar katika harakati zake za kukuza uchumi na kuimarisha
maendeleo.
Dk. Shein ameeleza
kuwa miongoni mwa juhudi zilizochukuliwa na Oman katika kuisaidia Zanzibar ni
pamoja na ujenzi wa Chuo cha Afya kilichopo Mbweni pamoja na fedha taslim kwa
ajili ya ununuzi wa vifaa vya Kiwanda cha Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali, msaada
wa gari kwa ajili ya viongozi wa Serikali na misaada mengine ambayo nchi hiyo
imeshawi kuitoa.

Post a Comment