UPELELEZI wa kesi ya mauaji ya kukusudia ya aliyekuwa Mjumbe wa
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi umekamilka,anaadika Faki
Sosi.
Mbele ya Thomas Simba Hakimu Mkazi Mkuu, Pamera Shinyambala wakili
wa serikali amedai kuwa upelele wa kesi hiyo umekamilika hivyo ameiomba
mahakama ipange tarehe kwa ajili ya kusikililiza maelezo ya mashahidi.
Miongoni mwa washtakiwa wanaokabiliwa na kesi hiyo ni
Chibago Magozi (32), John Mayunga (56),Juma Kangungu (29), Paulo Mdonondo
(30), Mianda Mlewa (40), Zacharia Msese (33), Msungwa Matonya (30) na
Ahmad Kitabu (30).
Wengine ni aliyekuwa mlinzi wa marehemu Dk Mvungi, Longishu
Losingo (29), dereva na mkazi wa Kitunda, Masunga Makenza (40), mkazi wa Tabata
Darajani, Paulo Mdonondo (30), mkazi wa Buguruni, Zacharia Msese (33) na mkazi
wa Mwananyamala, Ahmad Kitabu (30).
Kesi hiyo itaendelea tarehe 29 Disemba mwaka huu.
Inadaiwa kuwa Kwa pamoja wanadaiwa hao Novemba 3, mwaka
2013, walifanya kosa hilo la mauaji kinyume na kifungu cha 196 cha sheria na
kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Post a Comment