0


        Imeelezwa kuwa, kuwepo kwa  taasisi  ya   tume  ya  maadili  ya viongozi wa umma Zanzibar   kutasaidia kulinda  maadili  kwa  viongozi  pamoja  na  wananchi  wake.
 Mwenyekiti wa tume  ya  maadili  ya viongozi wa umma Zanzibar Asaa Ahmad Rashid 



        Mwenyekiti wa tume hiyo Asaa Ahmad Rashid ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Shangani mjini Zanzibar, amesema kuundwa kwa tume hiyo ni moja kati ya malengo ya Serikali na kuunda taasisi tofauti za uwajibikaji na utawala bora.
Ameyataja baadhi ya  majukumu  ya  tume  hiyo kuwa ni pamoja na kupokea  malalamiko  kutoka  kwa wananchi  kuhusiana  na  suala  la  uvunjifu  wa maadili lakini  pia  kukuza uelewa  wa  maadili  kwa  viongozi  na wananchi.
        Pamoja na hayo Asaa ameweka wazi kuwa tume hiyo imeweka adhabu ya kukatwa mshahara, kushushwa cheo, kusimamishwa kazi, kustaafishwa, kuondolewa madarakani au kufukuzwa kazi kwa kiongozi wa umma atakaekiuka maadili yaliyowekwa na tume hiyo.
        Kwa mujibu wa utaratibu wa tume hiyo, mwezi Disemba kila mwaka viongozi wa umma wanatakiwa kujaza fomu maalumu ya tume hiyo na kuirudisha.
Tume  hiyo  imeundwa  na  mwenyekiti  na  makamishna  wawili  akiwemo  Said  Bakari  Jecha na Sebtuu  Mohammed  Nassor.

Post a Comment

 
Top