0
abiria watwangana ndani ya mwendokasi DAR
Kuna msemo unaosema Uzee mwisho Chalinze, msemo uliovuma sana kipindi cha nyuma hata hivyo msemo huo umeweza kujitokeza tena mchana wa jana 23 Desemba baada ya kutokea tafrani ndani ya basi la Mwendokasi (UDART) kwa wazee wawili kupishana kauli na kisha kuamua kushikana mashati.
Tukio hilo la aina yake, lilinzia kituo cha Magomeni Morocco ambapo abiria hao waliopandia basi lao hilo katika kituo hicho cha Magomeni kwa mmoja wapo kumkanyaga mwenzie na hali ikabadilika ghafla na kuanza kushikana mashati na kupigana
Wazee hao kila mmoja aliwa akimtambia mwenzie “Mimi huniwezi mtu wa mjini nimesoma mjini Azania Boys!” na Mzee Mwingine akajibu mapigo kuwa naye ni mtu wa mjini na amesoma mjini Tambaza Boys”.
Wazee ambao ni abiria na kila mmoja hakiwa na munkali, waliamua kuvaana na kuanza kupigana makonde hadi abiria wengie walipowaamulia.

Post a Comment

 
Top