0

Tokeo la picha la donald trumpTrump ataingia lini rasmi uongozini?

Ataapishwa siku ya Ijumaa tarehe 20 mwezi Januari mwaka 2017. Lakini kabla ya siku hiyo atatangaza timu yake, apewe taarifa za siri zikiwemo za siri, kuhusu usalama na oparesheni za kijeshi.

Trump ataishi ikulu ya White House?

Wakati wa mahojiano na mtandao moja mwaka uliopita, bwa Trump alionekana kuzima uvumi kuwa atakiuka tamaduni ya miaka mingi ya kuishi ikulu na hata mjini Washingto
Kwenye mahojiano hayo Trump alisema kuwa bila shaka ataishi kwenye ikulu.

Trump ataendelea kusimamia biashara zake akiwa Rais?

La hasha wakili wake amesema kuwa biashara zake Trump zitasimamiwa na watoto wake, Donald Junior, Ivanka na Eric.

Atasitisha utoaji mimba?

Mwezi Machi Donald Trump alisema kwa utoaji mimba unahitaji kuharamishwa na aliunga mkono aina fulani ya adhabu kwa wanawake ambao hutoa mimba. Lakini baadaye alionekana kulegeza kamba akisema kuwa suala hio linastahili kushughulikiwa na majimbo binafsi.
Trump amesema kuwa anaunga mkono marufuku dhidi ya utoaji mimba, isipokuwa ile inayokana na ubakaji na wakati maisha ya mama yako hatarini.


Nina bima ya afya chini ya mfumo wa Obamacare. Nitaipoteza?

Donald Trump ametaja wazi kuwa kuondoa mfumo nafuu wa Obamacare ndio itakuwa ajenda yake kuu , na anarajia kuuondoa haraka iwezekanavyo.

Ndoa za jinsia moja zitaendelea kutambuliwa?

Donald Trump amesema wakati wa mahojiano kuwa anapinga ndoa za jinsia moja licha ya yeye kudai kuwa ashahudhuria ndoa hiyo.
Amesema kuwa ni suala linalostahili kuamuliwa kwenye majimbo badala ya nchi nzima na alighadhabishwa na uamuzi wa mahakama mapema mwaka huu ambao ulihalalisha ndoa za jinsi moja kote nchini.
Lakini mapema mwaka huu alisema kuwa atawateua majaji wa mhakama ya juu kutupilia mbalia uamuzi huo.


Mimi ni muislamu, bado nitaruhusiwa kuenda likizo nchini Marekani?

Baada ya ufyatuaji mkubwa wa risasi mwaka uliopita mjini San Bernardino ambapo watu 14 waliuawa, bwana Trump alitaka waislamu wote wazuiwe kuingia nchini Marekani.
Matamshi hayo yalikosolewa kote duniani na hata kutoka kwa mgombea mwenza Mike pence ambaye aliyataja kuwa yanayokiuka katiba.
Miezi kadha iliyopita Trump ameonekana kuachana na mipango hiyo

Post a Comment

 
Top