0


bangi
Kamati ya ulinzi na usalama wilayani Tarime mkoa wa Mara imebaini na kuteketeza kwa moto mashamba saba ya bangi kwenye milima ya kijiji cha Wegita wilayani humo ikiwa ni mkakati wa wilaya hiyo wa kutokomeza kabisa kilimo hicho haramu ambacho kimekuwa kikiathiri nguvu kazi ya taifa.
 
Ilituchukua mwendo wa karibu saa matatu kuupanda mlima wa Wegita ulioko umbali wa kilometa nane ili kuyafikia mashamba makubwa ya bangi na baadae kuyafyeka na kisha kuyateketeza kabisa mazao hayo.
Baada ya kumalizika kwa zoezi la kufafyeka na kuyachoma mashamba hayo mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Tarime Bw. GLORIUS LUOGA akaelezea namna walivyofanikiwa kukomesha ulimaji wa zao hilo.

Post a Comment

 
Top