0

screen-shot-2016-11-11-at-7-45-05-am
Shughuli zote zikiwemo za uzalishaji katika mgodi wa Tanzanite One katika mji mdogo wa Merelani zimelazimika kusimama kwa zaidi ya saa sita baada ya wakazi wa kijiji jirani cha Naisinyai kukusanyika katika lango kuu la mgodi huo wakidai mwekezaji wa mgodi huo kukiuka makubaliano muhimu waliyojiwekea wakati akichukua mgodi huo.
 
Wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali na silaha za jadi  Wakazi hawa waliojawa na jazba bila kujali wala kuogopa mabomu ya polisi wanapiga kambi mbele ya lango kuu la kuingilia katika mgodi wa Tanzanite one kuanzia Majira ya saa kumi alfajiri wakidai, mwekezaji huyo kuwa ameshindwa kutekeleza kabisa hata moja ya makubaliano waliyojiwekea wakati akichukua mgodi huo  ikiwemo kuboresha huduma za kijamii katika kijiji chao ambazo ni maji, elimu na afya.
Licha ya jeshi la polisi kuimarisha ulinzi katika eneo hilo wakati wote wananchi hao  walifanikiwa kuzuia wafanyakazi wote kutoingia wala kutoka katika mgodi huo wakidai wanataka mwekezaji wa mgodi huo kufika eneo hilo.
Inserts……
Channel ten inalazimika kumtafuta moja ya wakurugenzi wa mgodi huo na haya ndo maelezo yake.
Mgodi huo kwa sasa unamilikiwa na Kampuni ya wazawa ya uchimbaji wa madini ya Sky Associates Group (LTD) ambayo ilinunua asilimia 50 ya hisa zilizokuwa zinamilikiwa na Kampuni ya Richland Resources ya Uingereza.

Post a Comment

 
Top