Matokeo ya ligi daraja la nne
inayoendelea wilaya ya Liwale mkoani Lindi hapo jana novemba 8 kulikuwa
na mchezo kali kati ya timu Polisi fc dhidi ya New generation mchezo
uliopigwa uwanja wa Halmshauri ya Liwale.
Mchezaji wa timu ya New generation akikimbia na mpira
mchezaji wa timu ya Polisi fc
Lango la timu ya Polisi fc lilivyoshambuliwa mara kwa mara
Katika mchezo huu kwa kila upande ulikuwa mgumu sana kutokana na kila
timu ilijipanga kutaka kupata ushindi au kutoa sare timu zote zilikuwa
zinashambuliana katika kipindi chote cha dakika 45 kipindi cha kwanza
lakini hakuna timu ilioweza kufumania nyavu ya mwezake.
Namo dakika ya 50 mchezaji wa Polisi fc,Lawrence Fusi aliipatia goli la
kuongoza goli lililowanyanyua mashabiki wengi kwa mashabiki wengi
waliiombea New generation ifungwe lakini matokeo yakabadilika baada ya
Salumu Mkeyenge kusawazisha goli katika dakika ya 89 na matokeo yakawa
sare kwa kufungana goli 1-1.
Kocha wa timu ya Polisi fc,Juma Lupia akizungumza na mwandishi wetu
alisema timu yake ilicheza vizuri na wachezaji wake walifuata maelekezo
aliowapa akiongeza katika mchezo ujao anatarajia kufanya vizuri nae
kocha wa timu ya New generation,Saidi Kachepa alikiri mchezo huo ulikuwa
mgumu huku akiwatupia lawama waamuzi wa mchezo huo na kuomba uongozi
kuondoa kasoro kwa upande wa waamuzi.
Matokeo ya mchezo wa novemba 7 kati ya Sido fc dhidi ya Nangando fc
ulimalizika kwa timu ya Sido fc iliweza kuibuka na ushindi mnono wa
magoli 5-0
Mchezaji wa timu ya New generation akikimbia na mpira
mchezaji wa timu ya Polisi fc
Lango la timu ya Polisi fc lilivyoshambuliwa mara kwa mara

Post a Comment