0
Aliko Dangote,mtu tajiri zaidi barani AfrikaAliko Dangote,mtu tajiri zaidi barani Afrika
Mfumuko nchini Nigeria huenda umeathiri kampuni ya Dangote Group inayomilikiwa na mtu tajiri zaidi barani Afrika Aliko Dangote.
Kampuni hiyo imeripotiwa kuwafuta kazi wafanyikazi 48 wakiwemo wataalam 36 wa kigeni na raia 12 wa Nigeria.
Ripoti zinasema kuwa hatua hiyo inatokana na gharama ya juu ya kufanya biashara katika taifa hilo na kampuni hiyo imeshindwa kupata fedha za kigeni kuwalipa wafanyikazi hao wa kigeni.
Lakini msemaji wa Dangote Group Tony Chiejina aliambia BBC kwamba ufutaji huo hauna uhusiano na mfumuko.
Kampuni hiyo inasema kuwa ilikuwa inaimarisha biashara zake na kwamba kazi zengine zimechukuliwa na kampuni tanzu.
Kampuni ya Dangote Group ni miongoni mwa kampuni zilizo na wafanyikazi wengi katika sekta hiyo.
Miezi miwili iliopita ,kitengo cha habari cha Bloomberg kiliripoti kwamba bwana Dangote alipoteza dola bilioni 5.4 mwaka huu kutokana na kuanguka kwa thamani ya sarafu ya Nigeria ,Naira.

Post a Comment

 
Top