Pep Guardiola aliibuka mshindi katika mechi ya
kwanza ya lingi kuu nchini Uingezea katika mechi iliyochezwa kati ya
Manchester United na Manchester City nyumbani kwa Man U huko Old
Trafford.
Kevin De Bruyne alifunga bao la kwanza la Man City
dakika ya 15 alipovamia ngome ya Manchester United na kumpata mlinzi
Daley akiwa usingizini.
Raia huyo wa ubelgiji pia alitoa mchango
mkubwa katika bao la pili na Man City, baada ya kumpa pasi safi Kelechi
Iheanacho ambaye aliutumbukiza mpira wavuni bila kuchelewa.
Iheanacho,
mshambuliaji raia wa Nigeria mwenye umri wa miaka 19, alisema anafuraha
sana kwa kuipa klabu yake bao la ushindi, na kuongeza imani yake mbele
ya meneja Pep Guardiola.
Post a Comment