SEHEMU
YA TISA
“Habari zako ninazo kijana wangu mapema tu nilipokea taarifa zako kutoka kwa mkuu wa kitengo chenu hapa chuoni pole sana kwa matatizo kijana wangu”, alisita kidogo huku akiendelea kunitazama nami nikiwa kimya kisha akaendelea kusema. “Maisha yana changamoto sana usimwamini mtu kabisa haswa hivi visichana vya hapa chuo.
Vinatamaa
sana havina mapenzi hata kidogo kijana wangu mimi ni kama mzazi kwako lazima
nikwambie ukweli kwasababu huku tumepitia sisi, nimefanya kazi hapa muda mrefu
hivyo maisha ya chuo kwa jumla usione umri wangu huu na wajua vijana wengi hapa
na maisha yao kwa ujumla”. Yule mkuu wa chuo aliongea bila kupepesa macho,
maneno ambayo yalikuwa ni kama mwiba
mkali kwangu. Ulikuwa mwiba kweli ambao ulinichoma na kutonesha kidonda changu
ambacho kilikuwa kinakaribia kupona kabisa.
Nilimtazama
kidogo, nikafumba funda la mate mdomoni mwangu kisha nikamkabili kwa maneno
ambayo nilijua yangeweza kubadilisha mada na kulekea kile nilichokuwa nimejia
ndani ya ofisi yake,. “Aahh… nimekupata mkuu vizuri sana, kwa sasa nimesahau
vitu vyote vya nyuma sasa naangalia maisha yangu maana familia inanitegemea”
nilimaliza huku nikiachia tabasamu la kinafiki kwenye mtazamo wake.
Mkuu
alinyamaza kimya baada ya maneno yangu, huku akishighulisha mikono yake kupekua
pekua mafaili fulani. Hata sikujua alikuwa anataka kunipa nini?,. Mara alitoa
karatasi ambayo ilikuwa ni form nakunipatia. Nilivyopewa nilijua niyakuomba
kurudia mwaka kutokana na kupitwa masomo.
Jambo lile nilishalitegemea kutokea sikuwa na wasi wasi, nilipokea kwa
moyo moja. Kabla ya kunipatia meelekezo juu ya form ile.
Tulitoka
nje mimi na Criss nilitulia kidogo nakuanza kuijaza ile form dakika chache
niliweza kuijaza vizuri kama inavyotakiwa. Nikamrudishia mkuu ambaye aliniambia nirudi
baada ya wiki ili ile form aipeleke mahali husika. Nilimwelewa mkuu vizuri kile
alichotakiwa kufanyika juu ya kuhakisha naendelea kupata elimu yangu.
Tulitoka
ofisini na kuanza kukatiza mitaa ya chuo taratibu mpaka ilipokuwepo darasa
ambalo nilikuwa nikisoma nilipiga hatua huku nikiwa nimeshika mkono Criss. Hatua
kadhaa tulifika darasani mule hakuna aliyeamini kila mwanafunzi wa darasa lile
alishikwa na nafuraha isiyo na kifani. Kila moja alifurahi kuniona tena nikiwa
kwenye afya njema kabisa hakuna aliyeamini juu ya ujio wangu katika nyakati
zile. Kutokana na kukubalika darasani
mule wapo baadhi ya wasichana walikuwa wakilia, vilio vya furaha. Si wasichana
tu walikuwa wanafuraha ajabu juu ya ujio wangu hata wavulana nawo nyuso zao
zilibeba furaha isiyo na kifani. Furaha ambazo kwa upande wangu niliziona za
kawaida maana wachache ndio walikuwa wakijitokeza nyumbani na hata kuwasiliana
nami juu ya afya yangu, hivyo niliona kama unafiki tu mbele ya macho yangu
lakini sikuonesha wazi wazi.
Nilichofanya
nikumchukua rafiki yangu Juma ambaye nilishampa mapema taarifa ya kuwa
ningekuwa pale, siku mbili nyuma.
Tulitoka nje huku tukiendelea kuzungumza, kiukweli
tulizungumza vitu vingi sana. Na hata Juma
hakusita kunigusia habari za Irine kipindi chote ambacho mimi nilikuwa sipo
vituko vyake.
Hakika
na kiri wazi hakuwa msichana ambaye mwanzoni nilidhani bwana ndio amepanga niwe
nae, nilimlaumu Mungu kunikutanisha na mwanamke yule huku nikiapa sitaweza kuwa
na mwanamke yule hata ingekuwa kwa kushikiwa mtutu.
Tabia
zake zilikuwa mbovu sana ndani ya chuo, kila mtu alifahamu nyendo za binti
yule. Namna ambavyo Juma alivyokuwa
akiniambia nilihusanisha na namna nilivyokuwa nikiingia chuoni pale kila mtu
alivyokuwa akiniangalia hapo nilifahamu vyema kwanini nilikuwa naangaliwa sana
hapo awali. Nilijuwa watu walikuwa wananisikitia kuling'ang'ania fupa ambalo
lilikosa mlaji, nilijiona mpumbavu muda wote kweli Irene hakuwa msichana wa
aina yangu kabisa hakustairi kupendwa na mimi. Juma aliendelea kuongea mengi
hakika alienda mbali sana,
“Ahahh.. hiiiiii”, niling'ata meno kwa hasira,
grafla nilisikia sauti ikiwa inaniita jina langu.
Sauti ile ilipenya kwenye ngoma zangu za masikio kudhihirisha ni jina langu lilikuwa likiitwa si mimi tu hata Criss mdogo wangu alikuwa akisikia sauti ile wakati nikiendelea kumsikiliza Juma.
Niligeuza
shingo yangu kuangalia ni nani alikuwa akiniita, kugeuka tu mboni zangu
zilikutana na taswira ya mdada ambaye sikuweza kumtambua vizuri hadi alipofika
mahali pale tulipokuwa mimi Juma na mdogo wangu Criss. Nilimfahamu kwa sura
jina lilikuwa limeshanitoka, ni muda mwingi na vile sikuwa sana na mazoea na watoto
wa kike, hivyo nilishamsahau jina lake ila sura haikuwa ngeni kabisa.
Muonekeano
wa yule binti baada ya kutufikia na kuanza kuzungumza nae niliona vyema hakuwa
anaamini ambacho anakiona mbele yake kamwe. Sura yake ilionekana imeshikwa na
mfadhahiko mbele ya macho yangu. Niliongea nae dakika chache na kutuacha pale
mimi na Juma tukiendelea kuongea jambo. Juma akanitupia swali, swali likaleta
dhahama kwenye kichwa changu.
Post a Comment