WAZIRI
wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametangaza
kuvifungia kwa muda usiojulikana vituo viwili vya Redio kurusha
matangazo yao.
Waziri Nape ametangaza uamuzi huo hivi
punde katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na
kuzitaja redio hizo kuwa ni Radio 5 FM ya Arusha na Radio Magic FM ya
jijini Dar es Salaam.
Amesema redio hizo kwa nyakati tofauti
na katika vipindi vyao tofauti walitangaza habari zilizokuwa na
uchochezi ambazo zinaweza kuvuruga amani ya nchi.
Aidha Nape amesema amewasiliana na
kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) ili kuwahoji
wahusika na kisha kushauri adhabu ambazo zitakazofaa dhidi yao.
Post a Comment