Askari
mmoja amepigwa risasi na kikundi cha watu kinachosadikiwa kuwa ni
Majambazi huko vikindu mkoa wa pwani muda huu, Kuna mapambano
yanayoendelea askari na kikundi hicho cha Majambazi wanarushiana risasi
hadi sasa.
Mapigano makali yanaendelea kati ya polisi na watu wanaosadikiwa kuwa
ni majambazi eneo la Vikindu, wilaya ya Mkuranga, mkoa wa Pwani.
Katika eneo la tukio tumeshuhudia magari ya polisi (defenda) zaidi ya
16 yakifika eneo la tukio huku polisi wakiwa wameshika silaha zao kwa
umakini mkubwa.
Post a Comment