Timu ya Kigamboni fc yaendelea kung'aa baada ya kuibuka ushindi wa goli 1
bila dhidi ya Kombaini fc katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa shule
ya Msingi muungano.
Goli pekee la kigamboni fc lililoipa ushindi lilifungwa na
Ramadhani mtunage goli liliofungwa katika dakika ya 25 kipindi cha kwanza na kupelekea mpaka
mchezo unamalizika dakika 90 matokeo yalikuwa Kigamboni 1 na Kombaini hawajapata kitu.
Kigamboni moja ya timu ambayo haijawahi kupoteza mechi hata moja toka waanze mashindano haya april 27 matokeo Likongowele 1-3 Kigamboni,may 5 Kigamboni 5-1 Nangando,may 11 Kombaini 0-1 Kigamboni huku ikisubiria mchezo mmoja kukamilisha mzunguko may 17 kutakuwa na mechi yao ya nne kati ya Z fc Vs Kigamboni.
Ligi hiyo ya Mbuzi vijana cup inayoendelea wilayani Liwale
itaendelea tena hapo kesho katika mchezo utakaokutanisha timu ya Kubota fc Vs
Wakaanga sumu fc.

Post a Comment