Abiria zaidi ya 300 wanaosafiri kutoka Liwale mkoani Lindi na wanaoelekea wilayani humo kutoka Dar es Salaam na maeneo mengine wamekwama kwa siku mbili njiani kufuatia ubovu wa barabara kuu inayoingia wilayani humo kuanzia Nangurukuru kufuatia magari kukwama kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini na hivyo kusababisha adha kubwa kwa watumiaji wa barabara hiyo.
Wakizungumza na ripota katika eneo la Zinga Kibaoni baadhi ya wasafiri hao
wamesema kuwa barabara hiyo imekuwa ni kero kubwa kwa wakazi wa Liwale
ambapo katika kipindi cha mvua imekuwa ni kawaida kulala njiani huku
nauli zikiwa juu na wamiliki wa magari kusitisha safari na hivyo
kuwasababishia usumbufu mkubwa.
Baadhi ya madereva wa magari yaliyokwama wakizungumzia tatizo hilo wamesema kuwa
changamoto ya barabara hiyo imekuwa ikiwagharimu sana na wamiliki nao wamekiri ya kwamba magari yanatumia gharama kubwa wanazotumia katika kutengeneza magari yao na
hivyo kuiomba serikali kuangalia uwezekano wa kutengeneza barabara hiyo
kutokana na umuhimu wake.
Naye Mkurugenzi wa halmashauri ya Liwale Gaudence Nyamwihura
akizungumzia na waandishi wa habari amekiri kuwepo kwa taarifa hiyo ambapo kwa
kushirikiana na mkuu wa wilaya Bw.Ephraim Mmbaga wamekwisha anza kuchukua hatua za
tahadhari kwa kuwashirikisha wakala wa barabara nchini Tanroads ili
kunusuru hali hiyo.
>>>ANGALIA PICHA ZINGINE KWA KUBOFYA HAPA
>>>ANGALIA PICHA ZINGINE KWA KUBOFYA HAPA



Post a Comment