Waziri
wa Kilimo,Mifugo na Uvuvui Mh.Mwigulu Nchemba sambamba na Mbunge wa
jimbo la Mvomero Mh Sadick Murad (mwenye shati ya drafti),ikiwemo na
Kamati ya Ulinzi na Usalama sambamba na wananchi wakishuhudia tukio la
mgogoro wa Wakulima na Wafugaji,ambapo takribani mbuzi zaidi ya 70
wamekatwa katwa mapanga na watu wasiojulikana,ambapo Waziri huyo
ameahidi sheria na hatua za kudumu za tatizo hilo kuchukuliwa haraka
iwezekanavyo.
Baadhi ya Mbuzi waliokatwa katwa na mapanga .
Waziri
wa Kilimo,Mifugo na Uvuvui Mh.Mwigulu Nchemba akiongozwa na wafugaji
kabila la Wamasai kufuatia mgogoro wao na Wakulima na kupelekea
uharibifu mkubwa wa kuuwawa kwa wanyama zikiwemo mbuzi zaidi ya 70.
Waziri
wa Kilimo,Mifugo na Uvuvui Mh.Mwigulu Nchemba sambamba na Mbunge wa
jimbo la Mvomero Mh Sadick Murad (mwenye shati la drafti),wakiwemo na
Kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya ya Mvomero na wananchi mbalimbali
wakishuhudia tukio la kuuwawa kwa mbuzi zaidi ya 70 wakiwa wamekatwa
katwa mapanga na watu wasiojulikana,ambapo Waziri huyo ameahidi sheria
na hatua za kudumu za tatizo hilo kuchukuliwa haraka iwezekanavyo.
Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvui Mh.Mwigulu Nchemba akiwahutubia Wananchi wa Wilaya ya Mvomero katika kijiji cha Dihinda mkoani Morogoro kufuatia mgogoro mkubwa kuzuka kati ya Wakulima na wafugaji,ambapo inaelezwa kuwa katika tukio hilo mbuzi na kandoo zaidi ya 70 wakiwa wamekatwa katwa mapanga na watu wasiojulikana.Waziri Mwigulu Nchema ameahidi kuwa sheria na hatua za kudumu za tatizo hilo kuchukuliwa haraka iwezekanavyo.
Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvui Mh.Mwigulu Nchemba akiwahutubia Wananchi wa Wilaya ya Mvomero katika kijiji cha Dihinda mkoani Morogoro kufuatia mgogoro mkubwa kuzuka kati ya Wakulima na wafugaji,ambapo inaelezwa kuwa katika tukio hilo mbuzi na kandoo zaidi ya 70 wakiwa wamekatwa katwa mapanga na watu wasiojulikana.Waziri Mwigulu Nchema ameahidi kuwa sheria na hatua za kudumu za tatizo hilo kuchukuliwa haraka iwezekanavyo.
February 9 2016 waziri wa kilimo, mifugo na uvuvi Mwigulu Nchemba alilazimika kusafiri haraka hadi mkoani Morogoro kijiji cha Kambala wilaya ya Mvomero,
baada ya taarifa za mapigano ya wakulima na wafugaji kumfikia, safari
hii yameingia kwenye headlines nyingine ya kuuwawa zaidi ya mifugo 75
kati ya mifugo 200 waliojeruhiwa kwa mapanga.
Waziri Mwigulu
amefika eneo la tukio na kuchukua hatua za haraka kwa kuagiza kamati ya
ulinzi ya mkoa na wilaya, kufanya uchunguzi na kuwatafuta wahusika wa
tukio la kukatwa katwa mapanga kwa zaidi ya mifugo 75, ili wafike mbele
ya mikono ya sheria nakuagiza mahakama kupitia upya hukumu
iliyotolewa mwaka 2015 ya kugawa mipaka kati ya eneo la wakulima na
wafugaji.
Mwisho waziri Nchemba
ameagiza uongozi wa mkoa na wilaya kufanya mkutano wa hadhara wa
wakulima na wafugaji tarehe 20/02/2016, ili kuanza harakati za kumaliza
mgogoro. Kati ya mifugo inayotajwa ni mbuzi, kondoo na ndama.





Post a Comment