Al shaabab waua polisi 2 Kenya
Polisi hao wanaaminika kuwa ndani ya gari lao wakishika doria katika barabara moja kabla yao kushambuliwa ghafla na wapiganaji hao
Wawili kati yao walipoteza maisha yao huku wengine wawili wakijeruhiwa vibaya.
Shambulizi hili la leo limetokea takriban kilomita 5 pekee kutoka pahala ilikoshambulia basi ya usafiri wa umma mapema wiki iliyopita na kuua watu wawili.
Vyanzo vya wapiganaji hao wa Al-Shabab pia vinadai kuwa walitekwa gari la kijeshi.
Dai hilo halijathibitishwa.
Hapo jana mtu anayeshukiwa kuwa mpiganaji wa Al Shabaab aliuawa alipokuwa akitega bomu la ardhini katika barabara hiyo yaLafey – El Wak.
Kundi hilo linadaiwa kuwa limegawanyika kuwa mawili baada ya baadhi yao kukubali kuungana na wanamgambo wa Islamic State.
Kundi hilo lililojitenga linadaiwa kuongozwa na Gamadhere aka Kuno wanaiunga mkono ISIS.
Mashambulizi haya yaliyochacha kwa mjibu wa Inspekta mkuu wa polisi nchini Kenya Joseph Boinett yanalenga kuwaonesha wadhamini wao kuwa wanauwezo wa kufanya masg=hambulizi ndani ya Kenya.
Kenya ilituma askari wake nchini Somalia mwaka 2011 ili kujaribu kushinda wapiganaji hao wa Kiislamu na kuisaidia serikali dhaifu.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.