Urusi imesema inashambulia makundi ya kigaidi Syria
Urusi, ambayo kwa mujibu wa mashahidi ilianzisha tena mashambulio Ijumaa, inasema inalenga IS.
Afisa mkuu wa Urusi anasema mashambulio hayo huenda yakaendelea kwa miezi mitatu hadi mine.
Alexei Pushkov, mkuu wa kamati ya mashauri ya kigeni katika bunge la Urusi, aliongeza kuwa Marekani ilikuwa tu “ikijifanya” kuangushia mabomu IS na akaahidi kwamba kampeni ya Urusi itafanikiwa zaidi.
Jeshi la angani la Urusi lilianza kushambulia maeneo ya Syria Jumatano.
Jeshi la Syria linasema Urusi ilitekeleza mashambulio 18 tangu Alhamisi jioni. Inasema baadhi ya mashambulio hayo yalitekelezwa Hama na Idlib, mikoa ambayo haina wapiganaji wa Islamic State kwa wingi.
Wizara ya Ulinzi ya Urusi ilisema ndege zake za kijeshi zilishambulia ngome ya IS eneo la Raqqa Alhamisi. Wanaharakati wanasema wapiganaji kadha wa IS waliuawa huko.
Mashambulio hayo ya ndege Syria ndiyo operesheni ya kwanza ya kijeshi wa Urusi nje ya eneo la uliokuwa Muungano wa Usovieti tangu kumalizika kwa Vita Baridi.
Onyo la mataifa ya muungano huo unaoongozwa na Marekani limetolewa huku viongozi wa Ufaransa na Urusi wakitarajiwa kukutana baadaye Paris.
Mkutano huo uliitishwa kujadili juhudi za kutafuta amani Ukraine, lakini sasa hilo huenda likagubikwa kwa Syria.
Upinzani nchini Syria umedai makundi ya waasi yanaompinga Rais wa Syria Bashar al-Assad, ambaye ni mshirika wa Urusi, nadiyo yanayoumizwa Zaidi na mashambulio ya Urusi.
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Urusi Sergei Lavrov, akiongea katika makao makuu ya UN New York, alisema Urusi itashambulia pia makundi mengine ya kigaidi likiwemo al-Nusra Front, lenye ushirika na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda.
"Hatuungi mkono kundi lolote. Tunapigana na ugaidi,” alisema.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.