0
Mahakama  ya  kimataifa  ya  uhalifu, ICC  leo  imewaambia majaji  wapitie  upya  uamuzi  wao  wa  kutoipeleka  Kenya katika  jopo  la  uchunguzi  la  mahakama  hiyo  kwa kushindwa  kutoa  ushirikiano  katika  kesi  dhidi  ya  rais Uhuru Kenyatta.
Waendesha  mashitaka  mwishoni  mwa  mwaka  2013 waliitaka  mahakama  hiyo  ya  ICC  kutoa  uamuzi  kwamba Kenya  ilishindwa  kuchukua  hatua  kuhusu  ombi  la upande  wa  mashitaka  kukabidhiwa  data za  kifedha  za Kenyatta, taarifa  za  simu  pamoja  na  nyaraka  nyingine wanazosema  zingeweza  kuthibitisha  kesi  ya uhalifu dhidi  ya  ubinadamu anaohusishwa  nao.
Waendesha  mashitaka  pia  wametaka  mahakama  ya ICC  kupeleka  suala  hilo  katika  chombo kijulikanacho kama   baraza  la  makundi  ya  kitaifa, chombo chenye wajumbe  kutoka  mataifa  123  na  linaloweza  kutafakari kuchukua  hatua.
Kesi  dhidi  ya  Kenyatta  ilivunjika mwishoni  mwa  mwaka jana  baada  ya  mwendesha  mashitaka  mkuu  wa  ICC Fatou Bensouda  kuondoa shutuma dhidi yake za  kupanga njama  za ghasia  baada  ya  uchaguzi  mwaka  2007-08 ambapo  zaidi  ya  watu 1,000 waliuwawa.

Post a Comment

 
Top