Wabunge wa Ujerumani wamepiga kura kuunga mkono mpango
wa tatu wa uokozi wa uchumi wa Ugiriki leo, licha ya idadi
kubwa ya wabunge walioasi miongoni mwa chama cha kansela Angela
Merkel, hali inayoashiria kwamba atapata taabu wakati atakaporejea
bungeni kuomba msaada zaidi kwa Uturuki.
Wakikubali wito wa waziri wa fedha Wolfgang Schaeuble kuipa Ugiriki nafasi ya kuanza kujijenga upya, wabunge wa chama cha kihafidhina cha CDU waliasi kwa idadi ndogo kuliko baadhi ya wanachama wa chama hicho walivyotabiri.
Mpango huo ulipitishwa bungeni kwa msaada wa chama cha Social Democratic, chama mshirika katika serikali ya kansela Angela Merkel pamoja na chama cha walinzi wa mazingira , The Greens, kwa kura 454, dhidi ya 113, na wabunge 18 hawakupiga kura.
Wakikubali wito wa waziri wa fedha Wolfgang Schaeuble kuipa Ugiriki nafasi ya kuanza kujijenga upya, wabunge wa chama cha kihafidhina cha CDU waliasi kwa idadi ndogo kuliko baadhi ya wanachama wa chama hicho walivyotabiri.
Mpango huo ulipitishwa bungeni kwa msaada wa chama cha Social Democratic, chama mshirika katika serikali ya kansela Angela Merkel pamoja na chama cha walinzi wa mazingira , The Greens, kwa kura 454, dhidi ya 113, na wabunge 18 hawakupiga kura.
Post a Comment