0



mwaandishi wetu Kilwa…….
Kikao cha baraza la madiwani katika halmashauri ya wilaya Kilwa mkoani Lindi kimeshindwa kuendelea baada ya  madiwani kugomea  kufanya kikao hicho kwa madai mbalimbali ikiwemo kushinikiza kulipwa posho zao zaidi ya miezi mitano.
Hali  hiyo ilijitokeza baada ya diwani wa kata ya Kilanjelanje Saidi Mtotela kuomba mwongozo kwa makamu mwenyekiti ambaye alikuwa anaongoza kikao hicho, juu ya posho , maslai na stahiki za  madiwani.
Baada ya hoja   hiyo kujibiwa na Mwanasheria wa halmashauri hiyo Godfray Jafari  kwa kuainisha aina za posho madiwani waliomtaka kaimu mkurugenzi Peter Mwelekela kutoa maelezo juu ya madai ya fedha zao za posho  za miezi  mitano wanayodai pamoja  na kiiunua mgongo chao kabla ya baraza kuvunjwa.
Abdala Mkumbaru diwani wa kata ya Chumu alisema kuwa hakuna haja ya kuendelea na baraza kama ofisi ya mkurugenzi haina majibu yakutosha juu ya malipo ya madeni ya madiwani hao.
Mkumbaru alisema kipindi cha madiwani kuwa madarakani kimebaki kifupi sana hivyo kama halmashauri hataweza kuwalipa katika kipindi hiki cha dakika za lala salama hawaweza kuzipata tena fedha
Diwani Haji Mulike alisema madiwani hawako tayari kuendelea na kikao hicho mpaka mkurugenzi  alipe madai yao  katika  kikao hicho  ndipo waendeleo  kufanya.
Mulike alisema kuwa watendaji wa halmashauri hiyo wamekuwa na dharau kwa madiwani na kuwasababishia madeni katika taasisi za fedha baada ya kushindwa kulipa madeni ya mikopo  ambapo kila mwezi ukatwa lakini hazifikishi benki kwa ajili ya kulipa madeni yao.
Alisema kuwa  kwa kipindi cha miezi zaidi ya mitano madiwani wamekuwa wakikatwa fedha za posho zao  kwa ajili ya kulipia madeni ya mikopo ya zaidi ya shs milioni 43 hazijalipwa hadi sasa.
Kwa upande  kaimu mkurugenzi mtendaji Peter Mwelekela aliwataka madiwani hao kuendelea na kikao hicho wakati zoezi la kuwalipa madeni yao linashughulikiwa   kiutekelezaji.
Kauli hiyo iliongeza vurugu hadi kumlazimu makamu  mwenyekiti wa halmashauri hiyo  Bakari Nalinnga kufunga kikao hicho  kwa kubadilisha tarehe ya kufanyika tena huku akiwaangiza watendaji wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanatafuta  majibu na fedha za kumaliza tatizo.

Post a Comment

 
Top