0

Image result for law


Mwaandishi wetu Lindi……
Afisa Mfawidhi tume ya haki za binadamu  Kanda ya Kusini Mourice Chisi  amewataka wasaidizi wa kisheria(paraligue)  kutumia nafsi zao kuwasaidia wananchi mkoani Lindi katika kutatua migogoro iliyochini ya uwezo bila kuleta mgongano na vurugu.
Wito huo ameutoa wakati alipokuwa anafunga  kikao kazi na kugawao vyeti kwa  wasaidizi wa kisheria kutoka wilaya za sita za mkoa wa Lindi  kilichoandaliwa na Kituo cha msaada wa kisheria wanawake na watoto mkoani Lindi  la LIWOPAC.
Chisi  alisema kuwa wasaidizi wa  kisheria ni watu  muhimu katika maeneo ya vijiji na mjini  ambako huduma za mahakama ziko mbali kwani kutokana uwezo wao  na uzoefu, ujuzi walionao  wanaweza  kufanya kazi za usaidizi wa  kisheria na kuweza kutataua  migogoro mbalimbali  katika jamii bila kufikisha mahakamani.
Nichukue nafsi  hii  kuwaomba wasaidizi wa kisheria kuwa waadilifu katika za kuwasaidia wananchi wanaokabiliwa  na migogoro mbalimbali na katika utetezi wa haki za wanawake , watoto na jamii kwa ujumla, alisema Chisi
Kwa upande wake mratibu   Kituo cha msaada wa kisheria wanawake na watoto LIWOPAC ,Cosma Bulu alisema  kikao  hicho ni kikao cha kazi   kwa wasaidizi wa kisheria cha kujadili  changamoto  na mafanikio  yaliyopatikana katika utendaji  kazi na kubadilishana uzoefu.
Bulu alisema kwa kipindi cha mwaka 2013/14  wasaidizi wa kisheria  wameweza kufanya kazi mbalimbali ikiwemo kutatua migogoro ya kijamii na kupunguza  wananchi kwenda  mahakamani kudai haki zao kwa kupeleka  kesi.

Post a Comment

 
Top