Mvutano
kati ya serikali ya Kenya na vyombo vya habari kuhusu kuhamia mfumo wa
digitali kutoka analogia ambao ulisababisha vituo vinne vikubwa vya
televisheni nchini humo kutorusha matangazo hivi sasa umeisha.
Vituo
hivyo vinne, ambavyo mfumo wake wa analogia ulizimwa, vitaanza kurusha
matangazo yake tena hii leo usiku kuanzia saa moja kasoro dakika kumi.
Makubaliano
hayo yalifikiwa siku ya Jumanne kati ya serikali na vituo hivyo vinne
vikubwa vya televisheni nchini Kenya NTV, QTV, KTN na Citizen TV ambavyo
vimekubaliwa kurusha matangazo yao jijini Nairobi chini ya mtandao wa
Africa Digital Networks (ADN).
Matangazo yao yatapatikana kwa wamiliki wote wa ving'amuzi visivyolipiwa kwa wakazi wa Nairobi na vitongoji vyake.
Post a Comment