Leo ni mwezi mmoja tangu wapiganaji wa Boko Haram waliposhambulia miji ya Baga na Doron Baga kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Idadi kamili ya watu waliokufa haijulikani lakini inadaiwa kuwa ni kati ya watu mia moja na hamsini hadi elfu mbili.Wakati wapiganaji wa Boko Haram wakivamia kutoka upande wa magharibi wa Baga, kundi la vijana waliodhamiria kupambana na kundi hili walijaribu kuulinda mji wao.
Yalikuwa mafanikio ya nadra kutokea dhidi ya Boko Haram. Kulikuwa na ahueni lakini haikudumu muda mrefu.
Ilikuwa taharuki. Wanawake na watoto, vijana na wazee walizikimbia nyumba zao na biashara, wengi wakikimbilia mji jirani wa uvuvi wa Doron Baga ulio ufukweni mwa Ziwa Chad.Boko Haram waliwafuata Doron.
Iwapo bunduki haikukudhuru, walianza kuua watu kwa kuwagonga na magari yao. Ufyatuaji wa risasi haukuchagua pa kulenga
Mauaji ya Baga na Doron Baga yalitokea mwezi mmoja uliopita…Boko Haram hawakusambaratishwa. Tangu wakati huo, waasi hao wameishambulia miji mingi zaidi kaskazini mashariki mwa Nigeria; watu wengi wamekufa na wengi zaidi wamelazimika kuyakimbia makazi yao.
Waziri wa Ujenzi Dkt.
John Pombe Magufuli amewahakikishia wakazi wa mji wa Tunduma mkoani
Mbeya kuwa Serikali itajenga barabara ya njia nne katika mji huo ili
kupunguza msongamano wa magari na kuuwezesha mji huo kuwa wa kisasa na
kibiashara.
Amesema hayo katika ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya barabara
inayoendelea katika mikoa ya Mbeya na Rukwa ambapo akiwa mjini Tunduma
amekutana na wananchi wanaofanyabiashara katika mji huo.
“Dumisheni umoja,amani na mshikamano ili mfanye biashara zenu na kukuza
uchumi nasi tutahakikisha tunajenga barabara ya njia nne ili kupunguza
msongamano wa magari na kuuwezesha mji wa Tunduma kuwa wa kisasa na
kibiashara na hivyo kuwa mahali pazuri pa watu kuishi”,amefafanua waziri
Magufuli.
Katika ziara hiyo waziri Magufuli amekagua mizani ya Nkangamo na
barabara ya Tunduma –Sumbawanga KM 225, iliyojengwa kwa kiwango cha lami
na kuwataka wananchi wa mkoa wa Rukwa kutumia barabara hiyo kukuza
uchumi wao na wa mkoa wao kwa kufanyakazi kwa bidii.
Akihutunbia wananchi wa Sumbawanga Waziri Dkt. Magufuli amewataka
wananchi kutambua kuwa barabara za lami zinajengwa kwa gharama kubwa
hivyo wazitumie kwa manufaa na wale walioko kwenye hifadhi ya barabara
wabomoe nyumba zao mapema ili kuwezesha ujenzi kufanyika kwa wakati.
Waziri Magufuli amesema Serikali iko katika hatua za awali kujenga
barabara ya Matai-Kasesha KM 50 kwa kiwango cha lami ili kuunganisha
mkoa wa Rukwa nan chi ya Zambia na hivyo kuvutia wawekezaji wengi
kuwekeza mjini Sumbawanga na hivyo kutoa fursa za ajira na uchumi kwa
wananchi.
Waziri Magufuli yuko katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya barabara
katika mikoa ya Mbeya,Rukwa,Katavi na Tabora ambako kuna miradi mikubwa
ya ujenzi wa barabara za lami inayoendelea.
Imetayarishwa na kitSengo cha habari na mawasiliano serikalini wizara ya
ujenzi.
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Post a Comment