0
Unamkumbuka Yakubu yule mshambuliaji Mnigeria, amerejea England na kujiunga na Reading.

Aliwahi kung’ara na Everton na Middlesbrough halafu akaamua zake kuondoka kwenda Qatar na kujiunga na Al Rayyan.

Kocha Steve Clarke wa Reading amesema wamemsajili kwa muda mfupi kama mchezaji huru.

Mnigeria huyo imeelezwa ana miaka 32 ingawa muonekano wake unaonyesha ana zaidi

Mara ya kwanza, Yakubu alitua England akitokea Maccabi Haifa akajiunga na Portsmouth kwa mkopo, hivyo ilikuwa mwaka 2003.

Post a Comment

 
Top