0


wajumbe wa baraza la madiwani  halmashauri ya wilaya kilwa mkoani Lindi wakiwa kikaoni cha bajeti





mwanasheria wa halmshauri ya wilaya kilwa na afisa utumishi wakiwa kwenye kikao cha baraza la madiwani wakifuatilia kikao hicho kwa umakini

 
Mwaandishi wetu Kilwa
 
Baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kilwa mkoa wa Lindi, lilipitisha mpango wa makisio ya bajeti mwenye jumla ya shilingi  bilioni 27.4 kwa  kipindi cha mwaka  wa fedha 2015/2016.

Akisoma bajeti hiyo Mkurugenzimtendaji wa halmashauri hiyo,Maimuna Mtanda alisema katika kipindi hicho halmashauri hiyo itahitaji kuwa na jumla ya shilingi 27,419,533,212.00 ambazo zitatumika katika kutekeleza miradi ya maendeleo na matumizi ya kawaida(mengineyo) na mishahara ya watumishi.
 Mtanda alisema  bajeti hiyo ina ongezeko la shilingi 6,420,907,082.00 sawa  na asilimia 30.6 ya bajeti ya  mwaka 2014/2015 kutokana na ongezeko la mishahara  yenye jumla ya shilingi 6403484812.00,sawa na asilimia 58.8 ya mishahara ya bajeti iliyopita,na ongezeko la mapato ya ndani lenye jumla ya shilingi 17,422,270.00.
Alisema kuwa fedha hizo zitatokana na makusanyo kwenye vyanzo mbalimba ikiwa ni pamoja na ruzuku ya mishahara shilingi 18,300,146,812.00,ruzuku ya matumizi mengineyo shilingi 1,617,843,000.00,ruzuku ya miradi ya maendeleo shilingi 3,161,080,000.00,mapato ya ndani shilingi 2,823,047,400.00 na misaada kutoka kwa wahisani na marafiki wa maendeleo shilingi 1,472,416,000.00
Mtanda alisema  ili kuongeza kiwango cha mapato ya ndani Halmashauri hiyo imeandaa mikakati ya ukusanyaji mapato,ikiwamo kuanzisha kikosi kazi cha ukusanyaji mapato,kuongeza wigo wa kubuni vyanzo vipya vya mapato,kuongeza viwango vya kodi katika baadhi ya vyanzo vya mapato na  kuimarisha rejesta za vyanzo mbalimbali vya mapato.
Mkurugenzi hiyo alisema katika matumizi ya shughuli za maendeleo kipaumbele kitakuwa kutekeleza miradi ya maji, kwani katika wilaya ya hiyo ni asilimia 47 ya wananchi  wanaopata na kutumia maji safi na salama
Kwa upande wake katibu  tawala msaidizi wa mkoa Lindi,Abdallah Dachi  aliitaka halmashauri hiyo kuwa na udhibiti na ukusanyaji wa mapato,ambapo pia aliitaka kuipa vipaumbele miradi ambayo haijakamilika(viporo)
Diwani wa lihimalyao Mahadhi Nangoma akichangia suala la makusanyo wa fedha za bima ya afya CHF katiak wilaya hiyo

Post a Comment

 
Top