Madiwani Nachingwea mkoani Lindi wakiwa kwenye kikao za bajeti
Tuwahurumie viongozi wa vitongoji na na vijiji , maneno ya Diwani wa Mnero mathew
Tuwahurumie viongozi wa vitongoji na na vijiji , maneno ya Diwani wa Mnero mathew
Afisa mipango wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi Mnunduma akiwa kwenye kikao cha madiwani cha bajeti
NACHINGWEA YAPAA
KUKUSANYA,KUTUMIA BILIONI 31 .7/-MWAKA 2016
Mwaandishi wetu Nachingwea
WAJUMBE wa baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya Nachingwea Mkoani Lindi limepitisha bajeti ya zaidi ya sh bilioni
31.7 zitakazokusanywa na kuelekezwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kipindi cha mwaka wa
fedha 2015/2016.
Kati ya kiasi hicho cha fedha,sh bilioni 2.237zinatarajiwa
kukusanywa kutoka kwenye vyanzo vyake mbalimbali vya mapato ya ndani ambapo ruzuku kutoka serikali
kuu na misaada kutoka kwa wafadhili ikitarajiwa kuwa ni zaidi ya sh bilioni
9.44
Akisoma taarifa ya mapendekezo ya mpango wa maendeleo na
bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea kwa mwaka wa fedha mwaka
2015/2016 katika mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo,Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Valery Kwembe alisema makadilio ya bajeti kwa mwaka wa
fedha wa 2015/2016 ni sh bilioni 31.762.
Alisema makadilio hayo yamepanda kutoka sh bilioni 22.568 kwa
mwaka wa fedha wa 2014/2015 ingawa hadi kufikia Novemba 2014,Halamashauri hiyo
ilifanikiwa kukusanya jumla sh bilioni 9.260 kati ya bilioni 10.080 zilizokusanywa
sawa na asilimia 92%ya makadirio.
Kwa mujibu wa Kwembe Halmashauri inatarajia kutumia bilioni
9.443 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kutumia vyanzo
mapato kama vile ruzuku kutoka serikali kuu,vyanzo vya ndani pamoja na fedha
kutoka kwenye programu za Elimu
Sekondari (SEDP),Maji na Usafi (NWSSP) ruzuru ya maendeleo ya serikali
za mitaa(LGCDG) Mpango shirikishi wa misitu(PFM)pamoja na Mfuko wa Barabara.
Kwembe alisema licha ya kupitisha makisio ya bajeti ya mwaka
wa fedha wa 2015/2016 Halmashauri hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali
ambazo huathiri utekelezaji wa malengo wa yanayowekwa kama vile kucheleweshwa
kwa fedha za ruzuku kutoka serikali kuu, pamoja kutofikiwa kwa malengo ya
ukusanyaji mapato kwenye baadhi ya vyanzo vya Halmashauri.
Kwa upande mwenyekiti wa halmsahauri hiyo Abdala Chikawe
aliwataka madiwani kushirikiana na watendaji katika kukusanya mapato kupitia vyanzo vya ndani vya halmashauri ili
kufikia malengo wajiojiwekea.
Chikawe
alisema kama madiwani na watendaji wa vijiji, na kata watashirikiana
katika kukusanya mapato kwa
uadilifu katika maeneo hayo kutaweza kusaidia kuongezeka kwa mapato ya
halmsahuri hiyo.
Post a Comment