0

 
mwaandishi wetu Liwale……
Wakulima wa wilayani liwale wameiomba serikali kuvitumia vyama vya ushirika kusambaza pembejeo za ruzuku ili kupunguza urasimu  na kuchelewa kuwafikia wakuilma kwa wakati unaofanya  na mawakala wanao sambaza kwa wakulima.
Ombi hilo metolewa  na wakulima wa korosho wa chama cha ushirika Mida  kata ya mihumo wilayani Liwale mkoa Lindi wakati walipokuwa wanazungumza na timu ya waandishi wa habari waliotembelea chama hicho .
Akizungumza kwa niaba ya wajumbe wa bodi ya ushirika ya chama hicho  Rashidi mpuke na Tabia Mbanila  alisema kitendo cha mfuko wa kuendeleza zao la korosho kusambaza  pembejeo kuwatumia  mawakala kumechangia  wakulima kuchelewa kupata  pembejeo hizo na kwa kiasi kidogo tofauti na mahitaji ya wakulima
Rashidi Mpuke  alisema  msimu 2013/14 uzalisha ulipungua kutokana  na kuchelewa kwa pembejeo hali iliyotokana  na wakulima kuutegemea mfuko wa pembejeo  kuwasambazia mpembejeo hizo kwa wakati.
Tabia mbanila alisema kuwa  ukosefu wa elimu juu ya  mfumo wa stakabadhi ghalani ni moja ya chngamoto zinazowakabili wakulima wakorosho  na kusababisha kuilalamikia serikali  kuwa inawatelekeza wakulima hao.
Mbanila alisema kama serikali  ingetoa elimu juu ya mfumo matatizo mengine yangepungua kwani mfumo  kwa ujumla ni mzuri  na ni mkombozi kwa wakulima  wa mazao ya korosho.

Post a Comment

 
Top