0
mwaandishi wetu Liwale.
Chama cha kuuza na kununua mazao Umoja wilayani Liwale mkoani  Lindi kimeanza  kutekeleza mradi  wa kugawa mbegu za Alizeti  zenye thamani ya shs milioni 6  kwa wakulima   zaidi ya 700  kwa lengo la kuinua uchumi  kwa kulitumia zao hilo kuwa zao mbadala badala ya korosho na ufata .

 Hayo yamebainishwa  na  mwenyekiti wa chama  hicho Hasani Mpako wakati wa  hafla ya uzinduzi  wa mpango huo Uliofanyika  katika ukumbi wa Tengeneza wilayani  hapa mwi mwazoni mwa wiki hii.

Mpako alisema   wakati  wa utekelezaji  wa mradi huo  wakulima watafaidika kutokana na uwezeshwa wa kiteknolojia  ili kuweza kupata  mazao mengi  sambamba  na kupata mashine na utaalamu  wa  utayarishaji wa mafuta ya alizeti.

Alisema mradi huo utatekelezwa kwa hawamu ya kwanza  katika kata tatu za majaribio ambazo ni kata za Nangando, Liwale, na Likongowele ambapo  pamoja na mambo mengine kwa  lengo la kubaini na kupunguza vikwazo na changamoto  wanazozipata wakulima wa korosho ili waone  namna ya kutumia  fursa hiyo badala ya kuendelea kuilahumu serikali kwa kukosa soko  la zao la korosho ambalo limekuwa zao kuu lakini soko lake halina uhakika wa bei na bei yake ipo chini hivyo haileti tija kwa wakulima ukilinganisha na ghalama za pembejeo.

Post a Comment

 
Top